Featured post

KASISI FISADI : LUSAKA AZOMEWA BUNGOMA

 Wanyeji wa Bungoma wamemkemea Gavana wa Jimbo hilo Kenneth Makelo Lusaka. Katika maoni waliyotoa mtandaoni, wananchi wamempaka samli ya ufi...

Saturday, 23 July 2016

KISU CHA NAMWAMBA

Kutokana na hali ya kisiasa nchini, viongozi wengi kutoka katika eneo la magharibi ya nchi wamekerwa na kuchoka kutelekezwa na vigogo wanaojiamini kuwa ndio nguzo kuu katika chama cha ODM. Kabla ya uchaguzi wa mwaka wa 2013,Musalia Mudavadi alikuwa wa kwanza kujiondoa chamani kwa kusingizia kudunishwa na kunyimwa nafasi ya kutaka kuwania Urais badala ya Raila Odinga. Mwaka huu nao, kumeshuhudiwa msepetuko wa kutisha katika chama hicho. Alianza Paul Otwoma, akavua mikoba ya unaibu wa mwenyekiti wa chama hicho. Akaja jenerali mkuu, mtu ambaye alidhaniwa kuwa mhafidhina wa Raila Odinga. Mtu aliyekataa kuapishwa kwa jina la Rais ila akaapishwa kwa kumtaja Raila Odinga ambaye kulingana na ECK wakati huo, alikuwa amefeli na kuwa wa pili chini ya Rais mstaafu Mwai wa Kibaki. Ababu Namwamba. Mbunge wa Budalangi. Ikumbukwe kuwa, huyu ni jamaa aliyekuwa mkutubi wa Raila katika eneo la Magharibi, kuzisanya data za kura, kuzihifadhi kwenye maktaba ya ODM na vitabu hivyo, alivitoa wakati wa uchaguzi na kwa kweli, ikiwa wewe umefuatilia chaguzi mbili zilizopita, utakubaliana nami nikimwita mkutubi. Boni Khalwale, aliapa wakati mmoja kuwa hangewahi kupikwa kwenye chungu kimoja na jenerali na hata kusema kuwa, angepewa bunduki, angemzamisha bwana huyu. Yote, ni kwa sababu ya kumtetea, kumhusudu, kumsujudu na kumkasimu Raila kuwa simba wa eneo la magharibi na Nyanza kwa jumla. Ababu, alijitoa kwa vyovyote vile, hata kukosana na ndugu ili Raila Odinga ang'ae katika anga la magharibi.

Kwa kupigana huko, akajihakiki na kuona kuwa, ana uwezo wa kuaminiwa zaidi na kudai ukatibu mkuu wa chama hicho. Hapo ndipo kaa alipoanza kuinua gando. Ababu! Katibu mkuu! ODM! Hapana. Yaliyofuata ni MEN IN BLACK. Akapewa uongozi kwa kuhofia kuwa angesepa mapema. Akaukumbatia. Akarejelea mchezo wake kumtetea BABA yake/yao. Akawa tena kiongozi wa PAC. Kaa akainua gando tena. Akaitwa MOLE. Kisa! Anaegemea upande wa serikali saaaana. Baadaye akaondolewa kwa kudaiwa kuwa hafanyi makadirio ya matumizi pesa kwa njia bora. Kwa kuwa ni mtu aliyewatakia waliompigia kura mema, akaanza kufanya kazi na serikali. Ziara baada ziara katika ikulu kwa yale aliosema, kuzungumzia suluhu ya matatizo yanayomkumba mwanamlembe. Aliwaalika na kuhudhuria mikutano ya Rais na Naibu wake katika eneo la magharibi. Akaunda vuguvugu la wabunge wa magharibi waliloliita WESTERN COCCUS.Vuguvugu lililonuia kuwaleta wanamagharibi pamoja. Ziara ya Rais kule Mumias sugar company, alikuwapo. Mikakati ya kukifufua kiwanda cha Pan paper, alikuwa mhusika mkuu. Mikakati ya kuboresha kiwanda cha Kabras Sugar Company, alihusika. Vyote hivyo vikamweka katika kundi la fuko. Akaonwa kama msaliti. Wakasema AMEKULA VYA RUTO. Dhibitisho ya hayo? Jumba la kifahari na Ziara za nje ya nchi na mkewe.

Ngoma ikalia sana na hatimaye ikapasuka kiwambo. Huyo, akabeba vyake na kujiendea. Sababu za kuondoka zinajulikana na wengi, moja wapo ikiwa labda ya ;ivumayo haidumu. Amevuma saaana kule. LABDA. Mwenyekiti wa chama cha ODM kule Bungoma ambaye pia ni Mbunge wa Sirisia, meja John waluke, pia amepunga buriani chama hicho. Inasemekana kuwa, hata seneta wa Busia Amos Wako, anapanga vyake kwenye kasha lake, tayari kuwafuata wenzake. Labda, kati ya chama na wao, mmoja au wote ni simba wala watu, wakiliwa huwani?

Kando na ODM, uamuzi wake umempa nguvu kiongozi wa wachache katika seneti bwana Moses Wetangula ambaye amemwambia Raila kuwa, itafaa kabisa iwapo atamwunga yeye mkono katika uchaguzi ujao. Wetangula alisema katika mkutano wa hadhar katika kaunti ya Busia kuwa, eneo lake la magharibi lina wapiga kura wengi kuliko kinara yeyote katika CORD hivyo hakuna mjadala kuhusu atakayepeperusha bendera ya Urais. Kuna mnong'ono kuwa, Musalia Mudavadi na Weta watafanya mazungumzo ili mmoja wao awanie urais mwakani. Athari kuu ya Kisu cha  ABABU NAMWAMBA.

Kisu cha  ABABU NAMWAMBA.

No comments:

Post a Comment