BAISKELI
Baiskeli ya kwangu,
Yasikize yalo yangu,
Nilikuleta kwangu,
Sababu ya penzi langu,
Kipenda uwe wangu,
Usiwe ja kindoo,
Watu wakuzungushe-zungushe.
Ghala langu sasa,
Sijivune kwa sura,
Ukadhani ni chakula,
Kaogopa na masizi,
Kakataa kwenda mekoni,
Ati ni kuharibu sura,
Linunua sufuria hiyo,
Kakupa ikawa yako,
Siniue kwa njaa,
Ati wahifadhi sura.
Nilikuwa mbali mashambani,
Kamulika macho nyumbani,
Kamwona kapera na rungu,
Kabeba sukari mkononi,
Akaja na matamu maneni,
Ndo umpe kilicho mafichoni,
Baiskeli nakutegemea kweli,
Usinilinge jiwe kisogoni.
Hata uwe mweupe pe!
Au uwe mweusi ti!
Sijivune na kuringa la.
Dunia takuning'iniza juu,
Ulie machozi kupukupu
Dunia hii si tamu,
Sifikirie tu utamu,
Mhenga alishanena,
Mali ni makuyu
Baiskeli ya kwangu,
Yasikize yalo yangu,
Nilikuleta kwangu,
Sababu ya penzi langu,
Kipenda uwe wangu,
Usiwe ja kindoo,
Watu wakuzungushe-zungushe.
Ghala langu sasa,
Sijivune kwa sura,
Ukadhani ni chakula,
Kaogopa na masizi,
Kakataa kwenda mekoni,
Ati ni kuharibu sura,
Linunua sufuria hiyo,
Kakupa ikawa yako,
Siniue kwa njaa,
Ati wahifadhi sura.
Nilikuwa mbali mashambani,
Kamulika macho nyumbani,
Kamwona kapera na rungu,
Kabeba sukari mkononi,
Akaja na matamu maneni,
Ndo umpe kilicho mafichoni,
Baiskeli nakutegemea kweli,
Usinilinge jiwe kisogoni.
Hata uwe mweupe pe!
Au uwe mweusi ti!
Sijivune na kuringa la.
Dunia takuning'iniza juu,
Ulie machozi kupukupu
Dunia hii si tamu,
Sifikirie tu utamu,
Mhenga alishanena,
Mali ni makuyu
No comments:
Post a Comment