Featured post

KASISI FISADI : LUSAKA AZOMEWA BUNGOMA

 Wanyeji wa Bungoma wamemkemea Gavana wa Jimbo hilo Kenneth Makelo Lusaka. Katika maoni waliyotoa mtandaoni, wananchi wamempaka samli ya ufi...

Monday, 25 December 2017

KRISMASI NDUMBA!

Januari mosi,
Haupo hausikiki,
Haupo machi,
hadi juni,
Hausikiki julai,
hadi novemba mwishoni,
Mwanangu anisaili,
Utafika lini,
Krismasi?

Mwaka jana ulipokuwa,
tulifurahia ghaya,
Kuku walichinjwa,
sharubati tukanywa,
Chapati na shamrashara,
tukavaa mpya mpya,
Yote tuliyafanya,
ili wewe kukupamba,
Mwanangu anisaili,
Utarejea lini,
Krismasi?

Kutu kuu ya izraili,
Kwa hamu twakusubiri,
Ufike kwetu mastakimuni,
Tuvae vilivyofichika makashani,
Tule vilivyobanzwa makabatini,
Tulie vilivyofukiwa magodoroni,
Tulalapo kitandani,
Tulale si ka' zamani,
Ulipoadimika  usingizi,
Na mguso wa mkeangu laini,
Mkeangu anisaili,
Utafika lini,
Krismasi?

Ama  wewe mwizi mkuu,
Uliniibia wangu kuku,
Ukaiba bashasha zangu,
Kwa ugomvi na mkeangu,
Alitaka vazi kuntu,
avae katika  mashamshamu,
Aliniumiza sana wengu,
Aliponenena, 'acha nende zangu,'
Kwa takwale kulikufuru,
Akinisaili mwanangu,
Nitamhaada kuwa  huku,
Hutatia lako guu,
Krismasi!

Ingawa kanihadaa sineni,
karo ya shule sinani,
zafungua mwakani,
Wanangu wa' mgongoni,
Wanidai "baba, nitatiani begini"
Pesa sina sinani,
Sauti yanicheka akilini,
" mpumbavu kalaghaiwa hadharani,
Ulidhani ya siri hatutayabaini! "
Mwangu akinisaili,
Sijui nimwambieni,
Krismasi.

No comments:

Post a Comment