Alikinunua jumatatu,
Hakikuwa na udhaifu,
Kilikuwa sahifu,
Kiling'aa kama dhahabu,
Aendako hakukisahau,
Akilini alikidhukuru,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Iliwadia jumanne,
Akakipaka rangi tele,
Kilichongeka ja mshale,
Alikopita kilipendeze,
Harusi kilimpeleke,
Akakilia na mchele,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Jumatano kaski hiyo,
Kamwe hakuachana nacho,
Alitakiwa kwenye mahojiano,
Atafute kazi ya kipato,
Alikivaa kiatu hicho,
Mwishoni kaona kivuno,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Nikwambieje alhamisi,
Alipokaa nyumbani,
Hakukiacha asilani,
Alikitumia bila kujali,
Alikiendea msalani,
Akakanyagia na kinyesi,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Ijumaa kakanyaga bati,
Akielekea msikitini,
Mwanya ukajibuni,
Kwenye ya kiatu soli,
Ndani kikajaa maji,
Alipotembea matopeni,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Jumamosi kwenye soko,
USidhani alikipa kisogo,
Alikikimbilia penye zogo,
Na kukimbia penye sokomoko,
Kiatu kikajaa kokoto,
Soli ikampa mgongo,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Kanisani alilimatia,
Kiatu kilimchubua,
Mguuni aliumia,
Siku nzima alilia,
Hakuwa na cha kutia,
Kiatu chake kiliraruka,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Asingekuwa mzulufu,
Aliyejaa upumbavu,
Angevinunua viwili viatu,
Abadilishe kila siku,
Asikitumie kimoja tu,
Kilichompa maumivu,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Hakikuwa na udhaifu,
Kilikuwa sahifu,
Kiling'aa kama dhahabu,
Aendako hakukisahau,
Akilini alikidhukuru,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Iliwadia jumanne,
Akakipaka rangi tele,
Kilichongeka ja mshale,
Alikopita kilipendeze,
Harusi kilimpeleke,
Akakilia na mchele,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Jumatano kaski hiyo,
Kamwe hakuachana nacho,
Alitakiwa kwenye mahojiano,
Atafute kazi ya kipato,
Alikivaa kiatu hicho,
Mwishoni kaona kivuno,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Nikwambieje alhamisi,
Alipokaa nyumbani,
Hakukiacha asilani,
Alikitumia bila kujali,
Alikiendea msalani,
Akakanyagia na kinyesi,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Ijumaa kakanyaga bati,
Akielekea msikitini,
Mwanya ukajibuni,
Kwenye ya kiatu soli,
Ndani kikajaa maji,
Alipotembea matopeni,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Jumamosi kwenye soko,
USidhani alikipa kisogo,
Alikikimbilia penye zogo,
Na kukimbia penye sokomoko,
Kiatu kikajaa kokoto,
Soli ikampa mgongo,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Kanisani alilimatia,
Kiatu kilimchubua,
Mguuni aliumia,
Siku nzima alilia,
Hakuwa na cha kutia,
Kiatu chake kiliraruka,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi
Asingekuwa mzulufu,
Aliyejaa upumbavu,
Angevinunua viwili viatu,
Abadilishe kila siku,
Asikitumie kimoja tu,
Kilichompa maumivu,
Heri viwe viwili viatu,
Visaidiane kwenye kazi

Nice one hii inaongelea mini labda yenye nafikiria sio hehe
ReplyDeleteVifungu vyenye mnato kweli labda yenye ninafikiria sio tupe uchambuzi wake
ReplyDeleteNikichambua nitapoteza utamu wake. Uzuri wa fasihi ni kuwa unaifasiri kwa mtazamo wako mwenyewe dada
Delete